Genesis 14:18-22

18 aNdipo Melkizedeki mfalme wa Salemu alipoleta mkate na divai. Alikuwa kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana. 19 bNaye akambariki Abramu, akisema, “Abarikiwe Abramu na Mungu Aliye Juu Sana,
Muumba wa mbingu na nchi.

20 cAbarikiwe Mungu Aliye Juu Sana,
ambaye amewaweka adui zako mkononi mwako.”

Ndipo Abramu akampa Melkizedeki sehemu ya kumi ya kila kitu.

21Mfalme wa Sodoma akamwambia Abramu, “Nipe hao watu na hizo mali uchukue wewe mwenyewe.”

22 dLakini Abramu akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua mkono wangu kwa Bwana, Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na dunia, na nimeapa
Copyright information for SwhKC